1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ouattara aapishwa rais wa Cote d´Ivoire

Mnette,Sudi/afpe7 Mei 2011

Rais Alassane Ouattara wa Cote d'Ivoire hapo jana aliapishwa rasmi rais wa taifa hilo, kufuatia miezi kadhaa ya vurugu za kisiasa.

https://p.dw.com/p/RMVT
Alassane Ouattara answers questions from journalists during a press conference at the Golf Hotel in Abidjan, Ivory Coast, Thursday, Jan. 6, 2011. Ouattara, the man recognized as the winner of Ivory Coast's recent presidential election, called Thursday for special forces from West African nations to remove Ivory Coast's incumbent president Laurent Gbagbo in a commando operation.(AP Photo/Rebecca Blackwell)
Rais wa Cote d'Ivoire, Alassane OuattaraPicha: AP

Ouattara, anaetambuliwa na jumuiya ya kimataifa kama mshindi wa uchaguzi uliofanyika nchini humo, hatimaye ameapishwa katika sherehe iliyofanywa katika makao ya rais mjini Abidjan, mji mkuu wa Cote d'Ivoire.

Wakati huohuo maafisa wamesema, rais wa zamani Laurent Gbagbo anatarajiwa kuhojiwa na mwendesha mashtaka wa serikali, katika mji wa kaskazini Korhogo, alikowekwa katika kifungo cha nyumbani.

Mapema wiki hii, Luis Moreno-Ocampo, mwendesha mashtaka mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, alisema kuwa ataomba idhini ya kuanzisha uchunguzi rasmi kuhusu uhalifu dhidi ya ubinadamu nchini Cote d'Ivoire.