1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Oliver Kahn atachukua nafasi ya Rummenigge Bayern Munich

Sekione Kitojo
30 Agosti 2019

Mlinda mlango nyota wa zamani wa  Bayern Munich Oliver Kahn ameteuliwa kuingia  katika bodi ya utendaji ya klabu hiyo kuchukua  nafasi ya mwenyekiti na mtendaji  mkuu Karl-Heinz Rummenigge mwezi Januari 2022.

https://p.dw.com/p/3OlEk
Oliver Kahn Fußball FC Bayern München
Picha: picture-alliance/dpa/A. Gebert

Mabingwa hao mara nyingi  nchini  Ujerumani wamesema  siku  ya Ijumaa (30.08.2019) kwamba  Kahn  mwenye  umri  wa  miaka 50 , nahodha  wa  zamani  wa  bayern  na  mchezaji  wa  kimataifa  wa Ujerumani, amesaini mkataba  wa  miaka  mitano  na  klabu  hiyo utakaoanza  Januari 1, 2020, baada  ya  kuthibitishwa katika mkutano  wa  bodi  ya  utendaji siku  ya  Alhamis.

Fußball | FC Bayern München | Oliver Kahn
Mlinda mlango wa zamani wa Bayern Munich Oliver KahnPicha: Bongarts/Getty Images/R. Orlowski

Kahn ambaye  hivi  sasa  anafanyakazi  kama  mfanyabiashara  na mtaalamu  wa  televisheni  katika  michezo, amekuwa  akifikiriwa kwa  kiasi  kikubwa  kuchukua  nafasi ya  Rummenigge  mwenye umri  wa  miaka 63, ambaye atajiuzulu wakati  mkataba  wake utakapofika  mwisho Desemba 31, 2021.

"Ni heshima  kubwa  kwangu kwamba nitaaminiwa  kushika wadhifa katika  ofisi kama  mwanachama  wa  bodi  ya  bayern Munich na baadaye  katika  ofisi  ya  mtendaji  mkuu CEO na  mwenyekiti wa bodi  ya  utendaji ya Bayern Munich," Kahn alisema  katika  taarifa.

Kahn mteule wa Hoeness

"Ningependa  kuishukuru  bodi ya uangalizi , ikiongozwa  na  Uli Hoeness, kwa  kuniamini."

Fußball | FC Bayern München | Oliver Kahn
Uli Hoeness(kushoto) meneja wa Bayern Munich alimpa siri fulani Oliver Kahn wakati wa mchezoPicha: Bongarts/Getty Images/A. Hassenstein

Kahn alikuwa  mteule aliyependelewa na  Hoeness, ambaye  binafsi anajitayarisha  kujiuzulu  kutoka  katika  medani  kuu  ya  Bayern Munich.

Siku  ya  Alhamis  rais aliyeitumikia  klabu  hiyo  kwa  muda  mrefu alisema  hataomba  kuchaguliwa  tena  hapo Novemba 15.

"Nina mahusiano  ya  karibu  na  klabu  hii na imejenga  maisha yangu," Kahn amesema. "Mafanikio ya kimichezo  na  kifedha, mshikamano na  mashabiki, uendeshaji  wenye  kuwajibika  kuelekea katika  historia  ya  klabu  hiyo na  maadili, hivi  ndivyo  Bayern inavyovisimamia."

Kahn alianza  kucheza  kandanda  akiwa  na  klabu  ya  karlsruhe kbla  ya  kuhamia  Bayern Munich mwaka  1994 na  kumtengeneza kuwa  mlinda  mlango nyota.