1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nini kinaendelea Chemnitz mashariki mwa Ujerumani?

Sekione Kitojo
31 Agosti 2018

Kwa mara  ya  pili  mfululizo waandamanaji  wenye msimamo mkali  wa  mrengo  wa  kulia  wameonesha chuki  yao kwa wageni  katika  mji  wa  Chemnitz.

https://p.dw.com/p/3476P
Chemnitz - Demonstranten mit einer Deutschlandfahne versammeln sich vor dem Stadion vom Chemnitzer FC
Picha: picture-alliance/dpa/R. Hirschberger

Polisi  wanaonekana  kuwa hawana uwezo tena. Baadhi  wanaonya, kwamba  hali  hiyo inatishia  kutapakaa  kila  mahali  nchini  Ujerumani. 

Si  mara ya kwanza  kwa  wageni kufanyiwa  mambo  haya  ya kukera.  Lakini  idadi  ya  waandamanaji  wa  mrengo  mkali wa kulia, na  kasi  iliyotumika  kuwakusanya, pamoja  na kulemewa  kwa  polisi  na kazi  ya  kudhibiti  maandamano hayo  mjini  Chemnitz  imewashitua  wengi. 

Kuanzia mwanzoni  mwa  miaka  ya  1990  kumekuwa  na wimbi  la  matumizi  ya  nguvu  dhidi  ya  wageni, na  sio hivyo  tu , lakini  kwa  kiasi  kikubwa  hali  hiyo  ilikuwa inatokea  katika  maeneo  ya  Ujerumani  mashariki. Katika mwaka  2015  baada  ya  kuingia  kwa  maelfu  ya wahamiaji matukio ya ongezeko  la  chuki  dhidi  ya  wageni. Tangu wakati  huo  hali  ya  hewa  imekuwa  ya  wasi  wasi.

Deutschland Sachsengespräch mit  Ministerpräsident Michael Kretschmer in Chemnitz
Waziri mkuu wa jimbo la Saxony Michael Kretschmer akizungumza na wakazi wa ChemnitzPicha: Reuters/H. Hanschke

Kitu  kilichozusha  hali  hiyo  mjini  Chemnitz  kilikuwa mapambano  yaliyosababisha  kifo  baina  ya  watu  kutoka mataifa  ya  kigeni na Wajerumani, ambapo  Mjerumani alichomwa  kisu  na kufariki. Mtu  anayeshukiwa  kufanya tukio  hilo  ni  Msyria  na  mtu  mwingine  kutoka  Iraq.

Kwa  hiyo waandamanaji  wa siasa  kali  za  mrengo  wa  kulia walitumia  tukio  hilo la  kuuwawa  kwa  mjerumani  kuwa  ndio sababu ya  kufanya  maandamano  na  kuchukua  sheria mkononi  mwao. Katika  vidio inaonekana , jinsi  gani waandamanaji  walivyowashambulia  wageni. Wanasema  sisi ni  wananchi , na  wengine  hata  wakisema, Wajerumani, jamii, taifa",  na pia  walionekana  wakitoa  salamu  za  enzi wa  utawala  wa  Hitler.

Kile  kinachoonekana  kutoka  Chemnitz  kinatisha kwasababu  taifa  linaonekana  kutokuwa  na  uwezo,  wageni, ama  wale wanaotakiwa  kuchukua  hatua , kutokana  na kundi  la siasa  kali  wanavyofanya.  Wanasiasa wameshitushwa. Mwenyekiti  wa  mkutano  wa  mawaziri  wa mambo  ya  ndani  Holger Stahlknecht, anaonya  kwamba iwapo  taifa  na  jamii  haitaweza  kuamua  hivi  sasa  dhidi  ya hali  inayotokea, kuna  jambo  linaweza  kutokea.

Berlin Demonstration gegen rechte Gewalt in Chemnitz
Maandamano ya kupinga machafuko ya mrengo wa kulia mjini Chemnitz Picha: Imago/snapshot/K.M. Krause

"Chemnitz inaweza  kuonekana  kesho  kila  mahali." Mtaalamu  wa  chama  cha  SPD  wa  masuala  ya  ndani Bukhard Lischka  anzungumzia  kuhusiana  na  hatari  ya kutokea  vita  vya  wenyewe  kwa  wenyewe  nchini Ujerumani. Na mwandishi  habari  Michel Friedman alisema wakati  akizungumza  na  DW, matukio  ya  Chemnitz ni tone tu katika  vuguvugu  la  chuki dhidi  ya  demokrasia. Limetawanya kundi hili mizizi katika  jamii, kuliko tunavyofikiria.

Demokrasia nchini Ujerumani ni thabiti, lakini katika baadhi ya maeneo haikidhi masharti ipasavyo kuweza kuthibitisha hilo.

Huko  nyuma mara  nyingi jimbo  la  Saxsony limekuwa katikati  ya  matukio. Juergen Kasek wa  chama  cha  Kijani katika  jimbo  la  Saxony  amekiambia kituo  cha  utangazaji cha  DW  kwamba,  "tumekuwa  na  matatizo  makubwa katika  jimbo  la  Saxony la watu wenye  siasa  kali  za mrengo  wa  kulia, kutoa  hukumu ya  bila  kuhakikisha mambo, ubaguzi, hali  ambayo  imekumbatiwa  na  watu wengi  katika  jamii.

Michel Friedman anaamini  kwamba jimbo  la  Saxony linakazi kubwa  ya  kufanya, kwa  kuwa  watu  wanashambuliwa  kwa kuwa  tu wanaonekana tofauti.

Mwandishi: Hasselbach, Christoph / ZR / Sekione Kitojo

Mhariri: Idd Ssessanga