Neymar ataka kuendelea kubakia PSG
25 Mei 2022Licha ya kushindwa kufikia thamani yake ya rekodi ya dunia ya euro milioni 222 kimchezo, hasa wakati ambapo kuna tetesi kwamba klabu hiyo bingwa ya Ufaransa iko tayari kumruhusu aondoke. Soma Neymar akaribia kujiunga na PSG
Neymar mwenye umri wa miaka 30 raia wa Brazil alitia saini kurefusha mkataba wake mwaka jana hadi mwaka 2025.
Hata hivyo, umekuwa msimu mbaya tena kwake kutokana na jeraha ambalo linaibua maswali juu ya siku zijazo katika klubu ya PSG.
soma Messi, Neymar, Mbappe hawakufua dafu
Gazeti la michezo la L'Equipe limedai kwamba PSG haitopinga Neymar kuondoka.
Nyota huyo wa zamani wa Barcelona alipachika wavuni bao lake la 100 kwa PSG tangu alipojiunga na klabu hiyo 2017, baada ya kuilaza Metz 5-0 Jumamosi iliyopita. soma Neymar afunga hat-trick kuizamisha Baseksehir
Bado nipo
Neymar amesema hajasikia fununu za yeye kuondoka PSG.
"Sijasikia kitu kama hicho, lakini kwa upande wangu ukweli ni kwamba nataka kubakia" aliambia tovuti ya Oh My Goal.
PSG baada ya kumshawishi nyota mshambuliaji Kylian Mbappe kusaini mkataba mpya na kuipuuza Real Madrid, wanalenga kujenga kikosi madhubuti wakiwa na matumaini ya kushinda ligi ya mabingwa barani Ulaya, Champions.
Kuondoka kwa mkurugenzi wa michezo kutoka Brazil, Leonardo na nafasi yake kuchukuliwa na mreno Luis Campos kumeonekana kuwa jambo ambalo limeathiri pakubwa nafasi ya Neymar PSG.
//AFP