1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NEW YORK:Umoja wa Mataifa watahadharisha juu ya hatari ya njaa katika eneo la Sahel

10 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CD4N

Mamilioni ya watoto wanakabiliwa na tishio kubwa la kufa njaa katika nchi zinazopakana na jangwa la Sahara.

Umoja wa Mataifa umetaarifu hayo na kueleza kuwa watoto milioni moja na laki mbili na nusu wenye umri wa chini ya miaka mitano hawapati chakula cha kutosha nchini Niger,Mali, Mauritania na Burkina Faso.

Umoja wa Mataifa umesema msaada wa haraka wa dola milioni hamsini unahitajika kwa ajili ya watoto hao katika nchi hizo.