NEW YORK:Bloomberg ajitoa Republican
20 Juni 2007Matangazo
Meya wa New York Michael Bloomberg amejitoa kwenye chama cha Republican nchini Marekani.
Hatahivyo meya Bloomberg hakutaka kusema chochote juu ya uvumi kwamba anataka kugombea wadhifa wa rais kama mgombea huru katika uchaguzi utakaofanyika mwakani nchini Marekani.