1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ndege iliyowabeba Mawaziri wa Ujerumani yapata tatizo

13 Aprili 2023

Ndege inayowabeba mawaziri wawili wa Ujerumani kwa ziara rasmi nchini Niger imepata tatizo dogo la kiufundi wakati wa kutua.

https://p.dw.com/p/4PzXF
Deutschland | Wunstorf | Rückkehr der Bundeswehr aus Afghanistan
Picha: Axel Heimken/AFP/Getty Images

Waziri wa ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius na mwenzake wa maendeleo Svenja Schulze wamewasili mjini Niamey kuanza ziara ya siku kadhaa katika eneo la Sahel.

Msemaji wa wizara ya ulinzi ameliambia shirika la habari la Ujerumani dpa kwamba, ndege ya kijeshi ya Ujerumani iliyowasafirisha bado inaweza kutumika lakini licha ya tatizo hilo.

Katika ziara hiyo ambayo haikutangazwa kabla kwa sababu za kiusalama , mawaziri wote wawili wanataka kujionea hali ilivyo katika eneo hilo kabla jeshi la Ujerumani, Bundeswehr, halijaondoka nchini Mali.

Serikali ya Ujerumani inapanga kuwaondoa zaidi ya wanajeshi wake elfu moja walio chini ya mpango wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa MINUSMA ifikiapo Mei mwaka ujao wa 2024.