Rais Vladimir Putin amechaguliwa tena kuiongoza Urusi kwa muhula mwingine wa miaka 6. China na Iran tayari zimekwishamtumia salamu za pongezi, lakini nchi za Magharibi bado zinasitasita. Putin amekuwa mtu mwenye nguvu zaidi katika siasa za Urusi kwa takriban miongo miwili sasa.