Kutoka uvaaji wa barakoa shuleni hadi kuwakosa na kuwatamani mabibi zao wanaowasimulia hadithi za kale kabla ya kulala, watoto wanataabika na hali mpya iliyojitokeza sasa katika maisha yao. Makala ya sura ya Ujerumani inaangazia jinsi watoto wa Ujerumani wanavyohisi kuhusu janga la corona na maradhi ya COVID-19, takriban miaka miwili tangu janga hilo lilipozuka. Msimulizi ni Josephat Charo.