1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nahodha wa Sea-Watch Rackete amuita Salvini "mbaguzi hatari"

Sekione Kitojo
6 Julai 2019

Carola Rackete,nahodha wa meli ya uokozi wa wahamiaji ambaye ametoka kizuwizi cha nyumbani nchini Italia ametetea hatua aliyoichukua na kumuita waziri wa mambo ya ndani wa Italia Matteo Salvini "mbaguzi" na mtu "hatari".

https://p.dw.com/p/3Lgs6
Italien Rettungsboot Sea-Watch 3 im Hafen von Lampedusa | Carola Rackete, Kapitänin
Carola Rackete nahodha wa meli ya Sea-WatchPicha: Reuters/G. Mangiapane

Matamshi  yake , kutokana  na  mahojiano jana  Jumamosi  na gazeti  la  kila  siku  la  Italia  La Republica, yameendeleza  uhasama na  Salvini , ambaye  amemueleza  Rackete  kuwa  ni  mhalifu pamoja  na  "Mjerumani mkomunist  tajiri  ambaye amedekezwa." Katika  jibu  lake , nahodha  huyo  anapeleka  shauri  mahakamani  la udhalilishaji.

Spontandemo für Solidarität mit Kapitänin Carola Rackete in München
Waandamanaji wakimuunga mkono Carola RacketePicha: Imago Images/Overstreet

"Nina  wasi  wasi  juu  ya  jinsi  Matteo Salvini  anavyotumia  maneno yake , kwa  jinsi  anavyoeleza  mawazo  yake  ambayo  yanakiuka haki  za  binadamu. Ni  mtu  hatari  lakini wote  wenye  mawazo  ya siasa  za  kizalendo  na  siasa  kali  za  mrengo  wa  kulia wako hivyo, kuanzia  chama  cha  UKIP  cha  Uingereza  hadi  chama  cha AfD  nchini  Ujerumani,"  amesema.

Alipoulizwa  iwapo  atamwalika  Salvini  katika  meli  ya  Sea-Watch 3, Nahodha  huyo   mwenye  umri  wa  miaka  31  alijibu haitawezekana  kwa  kiongozi  wa  Italia  wa  chama  cha  siasa  kali za  mrengo  wa  kulia  cha  Ligi kwasababu  Sea-watch ina sheria kali: haruhusiwi  mbaguzi ndani  ya  meli."

Italien Rettungsboot Sea-Watch 3, Solidarität mit Carola Rackete, Kapitänin
Mabango yakielezea mshikamano na Carola RacketePicha: picture-alliance/NurPhoto/A. Ronchini

Rackete  aliwachukua  wahamiaji 40 kwenda  katika  kisiwa  cha Lampedusa Juni 29, akikaidi  amri ya  Italia  kutoingia  katika bandari  hiyo. Anaendelea  kuwa  katika  uchunguzi  wa  kuvunja sheria  za  uhamiaji  za  Italia  na  anatarajiwa  kukabiliwa  na uchunguzi  wa  pili siku  ya  Jumanne.

Wahamiaji

"Katika  hali  hiyo  hiyo  ningeweza  bila  shaka  kufanya  hivyo hivyo  tena, lakini  natumai  kwamba  iwapo  kesi  kama  hii itajitokeza , mara  nyingine  maafisa  wa  Italia  watachukua  hatua haraka  na  kuzuwia  kesi  kama  hii  kutokea," aliliambia  gazeti  la Republica. Meli  ya  Rackete , Sea-Watch 3, iliwachukua  wahamiaji Juni 12 nje  ya  pwani  ya  Libya. Walibakia  katika  meli  yake  kwa zaidi  ya  wiki  tatu kwasababu  Italia, kwa  msisitizo  wa  Salvini , ilikataa  kutoa  ruhusa  ya  kutia  nanga meli  yake.

Italien | Matteo Slavini | Lega
Waziri wa mambo ya ndani wa Italia Matteo SalviniPicha: picture-alliance/dpa/AP/ANSA/A. Carconi

Nahodha  huyo  alisema  hatua  aliyoichukua  ilikuwa  muhimu kuleta changamoto ya  kisheria  kwa  sheria  ya  sasa  ya  Italia inayopinga  wahamiaji ikiongozwa na  Salvini. "Baadhi  ya  nyakati unahitaji  kuchukua  hatua  ya  kukaidi  sheria  na  uasi  wa  kiraia ili kuweza  kuimarisha   haki  za  binadamu  na  kuleta sheria  potofu mbele  ya  sheria," ameongeza.

Akiweka  uwiano na raia  kutotii  sheria  chini  ya  utawala  wa wanazi, aliongeza: "Nchini  Ujerumani  tunafahamu  kwamba  kulikuwa na  nyakati  za  giza ambapo Wajerumani  walifuata  sheria  na makatazo  ambayo  hayakuwa  mazuri: kwa  sababu  tu  kitu  fulani ni  sheria haina  maana  kuwa  ni  nzuri. Alikiri  hata  hivyo , "kosa  la maamuzi" kwa  kugonga  boti  ya  polisi  wa  forodha  wa  Italia wakati  akiegesha  meli  yake  kisiwani  Lampedusa, na  kulaumu kuwa  alikuwa  amechoka. Kikosi  hicho  cha  polisi  killikuwa kinajaribu  kumzuwia.