Mwanamke anayesimulia historia ya nchi yake kwa sanaa
Sanaa
Grace Kabogo
18 Septemba 2020
Dessie Kamkosera ni mwanamke mwenye umri wa miaka 78, umri ambao kwa wengi hawawezi tena kujishughulisha na chochote. Lakini moyo wa usanii ndani yake unamfanya asiweze kutulia na badala yake atumie michoro kutunza historia ya nchi yake ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.