Baada ya kulifungia gazeti la Mawio kuchapisha nakala ngumu ama mtandaoni kwa miezi 24 kuanzia jana alhamisi, Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Harrison Mwakyembe amesema gazeti hili halikusikiliza mwito wa serikali wa kutowaandika viongozi hao wastaafu na lilikiuka misingi ya uandishi. Lilian Mtono alifanya mahojiano na waziri Mwakyembe.