Musiala atarajiwa kurudi kikosini Bayern
16 Januari 2026
Matangazo
Kocha Vincent Kompany amesema Musiala yuko karibu kurejea kikosini na amekuwa akionyesha hali nzuri na maendeleo chanya tangu arudi mazoezini.
Musiala alivunjika mfupa na kuumia kifundo cha mguu Julai katika mechi dhidi ya PSG, na kurejea kwake ni habari njema pia kwa timu ya taifa ya Ujerumani kuelekea Kombe la Dunia.
Kompany amedokeza huenda Joshua Kimmich akarudi baada ya jeraha la kifundo cha mguu, huku Bayern ikikabiliwa na upungufu wa wachezaji wa beki wa kulia kutokana na majeraha ya Konrad Laimer, Josip Stanisic na Sacha Boey.