Msumbiji yakamata washukiwa kadhaa wa ugaidi
26 Juni 2018Matangazo
Akizungumza kwa mara ya kwanza hapo jana (Juni 25) kuhusiana na ghasia hizo zinazolikumba jimbo la Cabo Delgado, Rais Nyusi aliahidi kwamba vyombo vya usalama yatachukuwa hatua kali kuwatafuta watu wanaohusika na kundi hilo la siri ambalo limehusika na vifo vya zaidi ya watu 30.
Utajiri mkubwa wa gesi asilia uligundulika nje ya pwani ya jimbo hilo, lakini machafuko hayo yametilia shaka uwezekano wa kuchimba gesi.
Urusi na Marekani zilisema mapema mwaka huukwamba ziko tayari kuisaidia serikali ya Msumbiji kutatua tatizo la mashambulizi hayo.
Rais Nyusi alifichua kwamba miongoni mwa washukiwa waliokamatwa ni raia wa Msumbiji na pia wa kigeni.