1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mo Salah aonesha ishara nzuri za kupona

Sekione Kitojo
4 Juni 2018

Mshambuliaji wa Liverpool na timu  ya taifa  ya Misri Mohamad Salah  anaonesha  ishara  chanya  za  kupona kutokana  na  maumivu  ya bega   kabla  ya  kuanza  kwa michuano  ya  fainali  za  kombe  la dunia  mwezi  huu.

https://p.dw.com/p/2yvEM
Mohamed Salah
Mohamed Salah wa Liverpool akitoka uwanjani watika pambano dhidi ya Real MadridPicha: picture-alliance/AP Images/AP Photo/D. Vojinovic

Mshambuliaji  huyo  mwenye  umri  wa  miaka  25 alikamilisha  msimu  ambao  amekuwa  na  mafanikio makubwa  na  Liverpool, katika  hali  ya  kukatisha  tamaa wakati  alipotolewa  uwanjani  akiwa  ameumia   katika nusu  ya  kwanza  ya  mchezo  wa  fainali  ya  kombe  la Champions League  katika  kipingo  dhidi  ya  Real Madrid mjini  Kiev  Mei  26  mwaka  huu.

Mohamed Salah
Mchezaji wa Liverpool na Real Madrid Mohammed SalahPicha: picture-alliance/AP Images/AP Photo/D. Vojinovic

Salah  alishindwa  kushiriki  katika  mchezo  wa  majaribio dhidi  ya  Colombia  Ijumaa  iliyopita  ambapo  timu  hizo zilitoka  suluhu  bila  kufungana  katika  matayarisho  ya Mafarao  hao  kutoka  Afrika  kaskazini  katika  kombe  la dunia.

Misri inacheza  dhidi  ya  Ubelgiji  katika  mchezo  wao  wa mwisho  wa  matayarisho  siku  ya  Jumatano  kabla  ya kuanza  kampeni  yao  ya  kombe  la  dunia  dhidi  ya mahasimu  wao  katika  kundi  A  , Uruguay  hapo  Juni  15. Wenyeji Urusi  na  Saudi  Arabia  pia  wanashiriki  katika kundi  hilo.

Mchezaji  mkongwe  wa  Mexico  Rafael Marquez anatarajiwa  kucheza  michuano  ya  tano  ya  fainali  za kombe  la  dunia  baada  ya  kutajwa  katika  kikosi  cha mwisho  cha  wachezaji  23  cha  nchi  hiyo  na  kocha Juan Carlos Osorio  leo  Jumatatu. Mchezaji  huyo  wa ulinzi  mwenye  umri  wa  miaka  39  alikuwa  akilengwa  na wizara  ya  fedha  ya  Marekani  Agosti  mwaka  jana  kwa tuhuma  za  madawa  ya  kulenywa. Hata  hivyo  amepata ridhaa  ya  shirikisho  la  kandanda  na  atajiunga  na wakongwe  Antonio Carbajal, Gianluigi  Buffon  wa  Italia na  Lothar Matthaus  wa  Ujerumani  katika  kundi  la wakongwe  walioshiriki  fainali  tano  wakiwa  wachezaji.

Fußball Juventus Turin - Torhüter Gianluigi Buffon
Mlinda mlango nguli wa Italia Gianluigi BuffonPicha: picture-alliance/Sportphoto24/G. Maffia

Modric amsubiri Neymar Madrid

Na  katika  michezo  ya  majaribio , mlinda mlango  wa Uhispania  David de Gea  alifanya  makosa  na kusababisha  timu  ya  Uhispania  kutoka  sare  ya  bao 1-1 nyumbani  dhidi  ya  Uswisi  katika  mchezo  wa  kujipasha joto  kabla  ya  fainali  za  kombe  la  dunia  jana  Jumapili, katika  mchezo  ambao  wenyeji  Uhispania  waliutawala lakini  walishindwa  kutumia  hali  hiyo  kushinda.

Uhispania  inasafiri  kwenda  katika  kambi  yao  ya mazowezi  ya  Krasnodar  wiki  ijayo  na  itacheza  mchezo wake  wa  mwisho  wa  kujipasha  joto  katika  mji huo  wa Urusi  dhidi  ya  Tunisia  siku  ya  Jumamosi, kabla  ya kuwakabili  mabingwa  wa  Ulaya  Ureno  katika  mchezo unaosubiriwa  kwa  hamu  wa  kundi  B mjini  Sochi  Juni 15.

Champions League - Manchester United vs Sevilla
Mlinda mlango wa Uhispania David de GeaPicha: Reuters/J. Nazca

Mchezaji  wa  kati  wa  Real Madrid  Luka  Modric amemtaka  nyota  wa  Brazil  Neymar  kujiunga  na mabingwa  hao  wa  Champions League  baada  ya kubadilishana  jezi  na  mshambuliaji  huyo  kufuatia mchezo  wa  kirafiki  wa  kimataifa  kati  ya  Brazil  na Croatia  jana  Jumapili. Mshambuliaji  huyo  wa  Brazil  na Paris St. Germain  alipachika  bao  katika  ushindi  wa mabao 2-0  dhidi  ya  Croatia. gazeti  la  Uhispania  la Marca  liliripoti  mwezi  uliopita  kwamba  baba  wa mchezaji  huyo  na  mshauri  wake , Neymar Sr. ameiambia PSG  kuwa  mwanae  anataka  kuondoka  kutoka  klabu hiyo  haraka  iwezekanavyo, akisema  alikutana  na wakurugenzi  wa  Real Madrid  katika  mji  mkuu  wa Uhispania.

Nae kocha  wa  zamani  wa   Arsenal  Arsene Wenger anashauku  ya  kurejea  tena  katika  kazi  ya  kufunza soka  lakini  anachukua  tahadhari  kabla  ya  kujiingiza katika  changamoto ambayo  atakuja  juta , wakati  akipana kutatua  hali  ya  baadaye  ya  maisha  yake  katika  wiki zinazokuja.

UEFA Europa League 2017/18 Halbfinale | Atletico Madrid vs. FC Arsenal | Arsene Wenger
Kocha wa zamani wa Arsenal Arsene WengerPicha: picture-alliance/dpa/SPORTPIX.ORG.UK

Kocha  huyo  wa  zamani  wa  Arsenal  aliondoka  katika klabu  hiyo  baada  ya  kuitumikia  kwa  miaka  22 mwishoni  mwa  msimu  uliopita na  hadi  sasa  amekuwa akihusishwa  na  nafasi zilizowazi  za  vilabu  kadhaa.

 

Mwandishi: Sekione Kitojo / rtre / afpe /dpae

Mhariri: Josephat Charo