1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa Jukwaa la vyombo vya habari DW waanza Bonn

Sekione Kitojo
11 Juni 2018

Hali ya kutokuwa na usawa duniani  ni mada  katika  mkutano wa 11  wa Jukwaa  la vyombo  vya habari duniani unaoanza leoJumatatu (11.06.2018) mjini Bonn.

https://p.dw.com/p/2zGud
Impressions Global Media Forum 2018 | June 11
Picha: DW/R. Oberhammer

Washiriki 2000 wa kimataifa  watajadili , vipi  vyombo  vya  habari  vinaweza kubadilisha  hali  hiyo na  kuonesha kwa vitendo , jinsi  wanavyoweza  kufanya kupambana  na  hali  hiyo  ya  kutokuwa  na usawa. 

Opening ceremony | Impressions
Waandishi habari wakishiriki katika mkutano wa Jukwaa la vyombo vya habari la DW mjini Bonn 2018

Wakati viongozi  wa  kisiasa  na  kiuchumi, viongozi wa  vyombo  vya  habari, wawakilishi wa mashirika  yasiyo  ya  kiserikali na wataalamu wakifanyia  kazi kalenda  ya  shughuli zao  katika  mwezi wa  Juni , basi hutenga siku  tatu , kwa kuwa  shirika  la  utangazaji la  Deutsche Welle  linawakutanisha pamoja katika  mkutano  wa  Jukwaa  la  vyombo  vya  habari, GMF. Mwaka  huu kuanzia  tarehe  11  hadi  13 Juni jukwaa  hilo  litajishughulisha  na  mada ya harakati  za  dunia, hali ya kutokuwa  na  usawa  duniani.

Jukwaa  la  vyombo  vya  habari  duniani, Global Media Forum, limekuwa  sasa mkutano  mkubwa  wa  kimataifa  wa vyombo  vya  habari  unaofanyika nchini  Ujerumani kila  mwaka.  Wanatarajiwa  wageni  2000  kutoka  karibu nchi  120.  Mkurugenzi wa  DW Peter Limbourg  anauchukulia  mkutano  huu wa  Jukwaa  la  vyombo  vya  habari  kuwa  ni  jukwaa  la  kipekee  la kubadilishana  mawazo  baina  ya  waandishi  habari   kutoka  nchi  mbali mbali, pamoja  na  viongozi wa  vyombo  vya  habari  ambao  ni  washirika wetu  duniani  kote pamoja  na  watu  ambao wanapambana kuwa na uhuru wa  vyombo  vya  habari.

Mariya Gabriel (European Commission, Commissioner for Digital Economy, Bulgaria) and Peter Limbourg (DW, Director General, Germany)
Mkurugenzi wa shirika la utangazaji la DW Peter Limbourg(kulia) akiwa na kamishina wa EU wa masuala ya digitali Mariya Gabriel katika jengo la DW mjini BonnPicha: DW/R. Oberhammer

DW yaenea kila mahali

Na  msimamo  wa  mkurugenzi Limbourg ni  wazi , kwamba  Jukwaa  la vyombo  vya  habari  linaonesha  kila  mwaka ,  vipi Deutsche Welle  imeweza kuenea  kila  mahali.  Tunaweza  kujifunza  mengi  kupitia  mijadala  na kubadilishana  mawazo.

Taarifa  nyingi  hususan  kutoka  Pakistan  na  Bangladesh  pamoja  na  mataifa ya  Afrika, anaripoti  Verica Spasoviska ,  mwaka  huu  zinahusika  katika  kile kinachojadiliwa  katika  mada  za  mkutano  huu. 

Opening ceremony / Peter Limbourg (DW, Director General, Germany)
Ukumbi wa mkutano wa Global Media Forum katika jengo la DW mjini Bonn 2018Picha: DW/P. Böll

Karibu  waandishi  habari 100  kutoka  katika  mataifa  yaliyoendelea  na  yale yanayoinukia  kiuchumi wanashiriki  katika  mkutano  huo, kwa  msaada  mkubwa  wa  kufanyakazi kwa  pamoja  na  wizara  ya  mambo  ya  kigeni, anasisitiza  kiongozi  wa shughuli  za  mkutano  huo  wa  Global Media Forum, Guido Schmitz. Schmitz anaelezea  kuhusu  ushirikiano  wa  jukwaa  hilo  la  vyombo  vya  habari GMF na  jimbo  la  North Rhine Westfalia kuwa  ni  muhimu  kwa  mafanikio  ya mkutano  huo.

Opening ceremony / Hamid Karzai (Former President of Afghanistan, Afghanistan) in the audience
Rais wa zamani wa Afghanistan Hamid Karsai yupo katika mkutano wa GMF mjini BonnPicha: DW/P. Böll

Mada hii  ya  kutokuwa  na  usawa  duniani itakuwa  na  matukio  karibu 60 katika  mkutano  huu , ambapo  katika  kiwango  cha  wanasiasa  kwa  mfano atazungumza  kamishna  wa  Umoja  wa  Ulaya  anayehusika  na  masuala  ya digitali Mariya  Gabriel. Ama  pia kiongozi  wa  zamani  wa  Afghanistan Hamid Karzai, ambaye  hapo  kabla  katika  mahojiano  na  DW aliwahi  kutoa matamshi  ya  kutatanisha. Ambapo  alisema  Karzai alizitupia  lawama Pakistan  na  Marekani  kwa  matatizo yanayoikumba  nchi  yake. Pia anatarajiwa  kuzungumza mwandishi  habari  Yusuf Omar , ambaye ni mwanzilishi  wa  ripoti  kupitia  simu  ya  mkononi , na  ataeleza  vipi  simu  ya mkononi  inaweza  kupambana  na  hali  ya  kutokuwa  na  usawa.

Mwandishi: Matthias Hein / ZR /  Sekione  Kitojo

Mhariri:  Mohammed Abdul Rahman