1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mionzi ya nyuklia yavuja Fukushima

Martin,Prema26 Machi 2011

Haijulikani lini wahandisi wa Kijapani watafanikiwa kuzuia mionzi ya nyuklia inayovuja katika mtambo wa nishati ya nyuklia wa Fukushima nchini Japan. Hiyo ni kwa mujibu wa shirika la kimataifa la nishati ya nyuklia IAEA.

https://p.dw.com/p/RCtE
In this photo released by Tokyo Electric Power Co. (TEPCO), gray smoke rises from Unit 3 of the tsunami-stricken Fukushima Dai-ichi nuclear power plant in Okumamachi, Fukushima Prefecture, Japan, Monday, March 21, 2011. Official says the TEPCO temporarily evacuated its workers from the site. At left is Unit 2 and at right is Unit 4. (Foto:Tokyo Electric Power Co./AP/dapd) EDITORIAL USE ONLY
Mtambo wa nishati ya nyuklia wa FukushimaPicha: AP

Maafisa wa IAEA katika makao makuu, mjini Vienna wamesema kwamba mbali na vinu nambari 1 na 2, sasa data zinaonyesha kuwa hata katika mtambo nambari 3, kuna dalili za kuvuja kwa mionzi ya nyuklia.

Afisa mkuu wa IAEA anaehusika na masuala ya usalama wa nyuklia amesema, hatua kadhaa zinahitaji kuchukuliwa hata kabla ya kuanza kutathmini kiwango cha uharibifu uliotokea.

Japan / Naoto Kan / Ministerpräsident (Foto: AP)
Waziri Mkuu wa Japan Naoto KanPicha: AP

Hapo awali waziri mkuu wa Japan, Naoto Kan alisema kuwa bado kuna kazi kubwa sana ya kufanywa huko Fukushima .

Idadi ya watu waliopoteza maisha yao, kufuatia tetemeko kubwa la ardhi na tsunami nchini humo tangu majuma mawili yaliyopita, sasa imefikia 10,000 na watu wengine wapatao 17,000 bado hawajulikani walipo.