Thelma Mwadzaya anaangazia hali ya jaa la jiji la Nairobi lililopo mtaa wa Dandora pembezoni mwa mitaa ya Kariobangi, Korogocho na Baba Dogo na lilianzishwa mwaka 1977. Kwa sasa limejaa pomoni na taka zinasababisha madhara kwenye mazingira. Pamoja na juhudi za vijana wawili kuasisi mfumo maalum wa kukusanya taka unaowapa wateja fidia ya bidhaa za matumizi.