Tunatumia 'cookies' ili kuboresha huduma zetu kwako. Maelezo zaidi yanaweza kupatikana katika sera yetu ya faragha.
Ni katika umri wa miaka 18 tu, wasichana hawa wameona changamoto ya uhaba wa panya kwa ajili ya matumizi ya kisayansi nchini Tanzania na kuchangamkia fursa. Sasa kwa namna gani wameanza ufugaji? #MsichanaJasiri 23.04.2021 Nenda kwenye vidio
Hatua ya Rais wa Tanzania Samia Hassan Suluhu kutangaza nia ya kukutana na vyama vya siasa nchini humo imepokelewa kwa hisia mchanganyiko// Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imelaani na kuahidi kuwachukulia hatua za kinidhamu askari waliomshambulia nmwandishi wa habari// Umoja wa Mataifa wasikitishwa na mzozo wa Tigray// Chanjo ya Covid kuwafikia watu wote Ujerumani kufikia mwezi Juni. Nenda kwenye sauti
Makala ya Wanawake na maendeleo inawaangazia Dr. Najat Kassim Mohammed, Profesa Eunice Mureithi na Dr. Margaret Samiji ambao wanaendesha kambi ya wasichana ya sayansi kwa wanafunzi wasichana nchini Tanzania. Wakati huo huo watalaamu hao wamewahimiza wanawake wajikite kwenye masomo ya sayansi na teknolojia. Nenda kwenye sauti
Mauaji ya George Floyd yaliyotokea mwaka jana na kufuatiwa na maandamano kwa ujumla vilisababisha wimbi la mageuzi kwenye jeshi la polisi kwenye majimbo mengi nchini Marekani// Wanaharakati wa wanawake nchini China wamekumbwa na wimbi jingine la ukandamizaji// Nchi inayoongoza katika kasi ya maambukizi ya virusi vya corona duniani kila siku, India, inaelekea kutumbukia katika mzozo mkubwa.
Ujerumani inatarajia kutoa chanjo ya corona kwa wananchi wote kufikia mwezi Juni. Canada yazuia ndege zote kutoka India na Pakistan kutokana na ongezeko la maambukizi ya covid. Viongozi mbalimbali wamewasili nchini Chad kushiriki mazishi ya Deby licha ya kitisho cha usalama.
Ni bustari maarufu huko Nairobi, Kenya iliyoboreshwa na kikundi cha jamii cha mazingira KECC. Sasa inavutia wakati awali ilikuwa eneo lililojaa uchafu na mahali pa kuogofya. Baada ya kuboresha mazingira, sasa watu wanafurahia mazingira safi na kuitumia kama mahala pa kupumzikia.
Rais Samia ametubia bunge la Tanzania na kutoa dira ya serikali ya awamu ya sita// Rais wa Marekani Joe Biden ameahidi kupunguza hadi nusu, kiwango cha gesi chafu kinachozalishwa na nchi yake ifikiapo mwaka 2030// Rais wa Jamuhuri wa Kidemokrasia ya Kongo Félix Tshisekedi alifanya mazungumzo na mwenzake wa Kenya, Uhuru Kenyatta jijini Kinshasa.
Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amelihutubia Bunge mjini Dodoma ikiwa ni mara ya kwanza tangu alipoapishwa mnano Machi 19, 202. Kwa mengi zaidi kuhusiana na hotuba hiyo iliyosubiriwa kwa hamu kubwa Babu Abdalla amezungumza kwa njia ya simu na mwandishi wetu Deo kaji Makomba kutoka mjini Dodoma. Sikiliza.
Makala ya Sura ya Ujerumani safari hii imejikitita katika kuangazia sera ya chama cha KIjani (watetezi wa mazingira) nchini Ujerumani pamoja na mgombea wao wa nafasi ya ukansela Annalena Baerbock mwenye umri wa miaka 40 kuelekea uchaguzi mkuu wa Ujerumani Septemba mwaka huu.
Tanzania imeendelea na mchakato wa kuwaandikisha wakimbizi wa Burundi waishio nchini humo ili kuwarudisha nyumbani kwa hiyari katika kambi zake za mkoani Kigoma. Mchakato huo unaendelea huku baadhi ya wakimbizi wakiwa hawana utayari wa kurejea nchini mwao.
Kenya kutuma wanajeshi DRC kupambana na ugaidi/ Hali shwari N'djamena kabla ya mazishi ya rais Idriss Deby/ Maadhimisho ya siku ya kuienzi Dunia/ Umoja wa Mataifa waonya juu ya kitisho cha njaa Myanmar
Polisi mjini Berlin, Ujerumani jana jumatano 21.04.21 walikabiliana waandamanaji wanaopinga sheria mpya ya kupambana na virusi vya corona iliyopitishwa na bunge. Ni sheria inayoipa serikali ya Kansela Angela Merkel mamlaka zaidi ya kupambana maambukizi ya virusi vya corona.
Makala Yetu Leo inatupia jicho mchango wa wadau mbalimbali wa jamii ya Kizanzibari kwenye kuyafanya Maridhiano kuwa na uhalisia maishani mwao na hivyo kuyasimamisha na sio kuyaangusha. Msisitizo ukiwa ni ujenzi wa Maridhiano ya Wazanzibari, suala lililoanzia uundwaji wa serikali ya pamoja. Salma Said na mengi zaidi
Kenya sasa imejiunga na mataifa 3 barani Afrika yanayotumia mtandao wa kasi na kuaminika wa 5G.Mauritius,Namibia na Afrika Kusini ndio walioitangulia.Jee mtandao wa 5G utaleta tija na kubadili maisha kivipi? Jibu na maengine mengi ni kwenye makala ya Sema Uvume. Sikiliza
Unapoulizwa swali kama kawaida ni muhimu kumakinika na kama hujaelewa basi usikurupuke tu. Ni Kiulizo Time na kama kawaida Masanja Mkandamizaji amekuwa mitaani na swali lake safari hii ni kuhusu kile anachokiita 'Pamba stick'. Hebu nawe jaribu kulijibu swali lake.
Sikiliza Dunia Yetu Leo Asubuhi kutoka Idhaa ya Kiswahili ya DW.
Sikiliza Taarifa ya Habari za Ulimwengu kwa Asubuhi ya 22.04.2021 kutoka Idhaa ya Kiswahili ya DW.
Waasi Chad wadai kusogea mji mkuu wa N'Djamena/ Derek Chauvin: Majaji wasema hukumu yake inatarajiwa kutolewa ndani ya kipindi cha miezi miwili na anakabiliwa na kifungo cha hadi miaka 40 gerezani> Mahojiano/ Kenyatta ziarani Congo/ Ujerumani: Serikali kuu kuongoza vita dhidi ya COVID-19/ Putin awaonya wanaoingilia masuala ya ndani ya Urusi
Maelfu ya watu Marekani wamepongeza uamuzi wa majaji 12 ambao umemtia hatiani polisi wa zamani wa Minneapolis kuhusiana na kifo cha Mmarekani Mweusi George Floyd. Hata hivyo wanasema safari ya kutafuta haki kamili bado ni ndefu.