Marekani yaimarisha ulinzi Ujerumani
21 Aprili 2007Matangazo
BERLIN:
Marekani imeimarisha ulinzi katika vituo na zana zake nchini Ujerumani.Miongoni mwa vituo hivyo, ni afisi zake ndogo za ubalozi-consulates na imewataka wamarekani waishio Ujerumani kuwa macho.
Si wakuu wa Marekani wala wa Ujerumani, waliotoa taarifa wazi juu ya hatari iliopo.
Magazeti ya ujerumani hatahivyo, yameripoti kuwa wairaki wenye siasa kali wamekuwa wakiangaza-angaza katika vituo vya Marekani viliopo Ujerumani.