1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yaimarisha ulinzi Ujerumani

21 Aprili 2007
https://p.dw.com/p/CC8S

BERLIN:

Marekani imeimarisha ulinzi katika vituo na zana zake nchini Ujerumani.Miongoni mwa vituo hivyo, ni afisi zake ndogo za ubalozi-consulates na imewataka wamarekani waishio Ujerumani kuwa macho.

Si wakuu wa Marekani wala wa Ujerumani, waliotoa taarifa wazi juu ya hatari iliopo.

Magazeti ya ujerumani hatahivyo, yameripoti kuwa wairaki wenye siasa kali wamekuwa wakiangaza-angaza katika vituo vya Marekani viliopo Ujerumani.