1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maoni: Matumaini yatokanayo na diplomasia kuhusu Libya

Sekione Kitojo
20 Januari 2020

Mwishoni mwa juma kulifanyika mjini Berlin nchini Ujerumani mkutano mkubwa wa upatanishi baina ya serikali inayotambuliwa kimataifa  nchini Libya na mbabe wa kivita upande wa mashariki mwa nchi hiyo Khalifa Haftar.

https://p.dw.com/p/3WUCa
Deutschland Libyen-Konferenz in Berlin
Picha: Reuters/A. Schmidt

Kwa muda mrefu Ujerumani imekuwa ikihangaika kutaka  kuchukua nafasi  ya  kuwajibika kimataifa.  Mara  nyingi  haiko wazi, iwapo hilo si  suala linalobishaniwa. Je uwezo wa kijeshi ni  mbaya. Nafasi za Ujerumani  na  urithi  wa  historia yake inaifanya  iwe katika nafasi  finyu sana. Lakini bila shaka, nguvu za Ujerumani zinaweza kusaidia  kwa  kuitazama  hapo zamani pamoja  na  uwezo wake wa kidiplomasia. 

Jana  Jumapili  Kansela  Angela Merkel  alikutana  mjini  Berlin na marais  wa  Ufaransa, Urusi , Uturuki na  Misri. Pia  mawaziri wakuu  wa  Uingereza  na  Italia. Waziri wa  mambo  ya  kigeni  wa Marekani, pamoja  na  wawakilishi wa  Umoja  wa  Falme  za Kiarabu, Umoja  wa  Ulaya  na Umoja  wa  Afrika. Libya  ambayo inapitia  katika  mzozo  mkubwa, iliwakilishwa  na  pande  zote zinazohusika  katika  mzozo huo. Kiongozi  wa  serikali inayotambulika  kimataifa  Faiz al-Farraj  na  mbabe  wa  kivita jenerali Khalifa  Haftar ambaye anadhibiti  sehemu  kubwa  ya ardhi  ya  nchi  hiyo.

Lakini  tukio  la  kuwapo katika  mkutano  huo viongozi wote  wanaohusika  katika  mzozo huo, bila  ya  wao  kukutana ana  kwa  ana  lina maana  kubwa kuhusiana  na  hali  ya  mzozo nchini  Libya. Tangu  pale alipoangushwa  kutoka  madarakani kiongozi  wa  muda  mrefu  wa Libya,  Mouammar Gaddafi,  mwaka 2011, nchi hiyo inajikuta katika  vita vinavyoendelea, ambamo mataifa  kadhaa  ya  nje yanahusika.

Kommentatorenfoto Jens Thurau
Jens Thurau, aliyeandika uhariri huuPicha: DW

Hapa  kuna  masuala  ya  mafuta na  gesi  na wakimbizi, ambao wahalifu  kutoka  nchini  Libya wanasaidia  kuwasafirisha  kupitia bahari  ya  Mediterania, ama kuwashikilia  nchini  Libya katika  hali  mbaya  kabisa.

Na  pia  kuna  suala  la ugaidi wa  makundi  ya  Kiislamu. Mchanganyiko  wa  vurumai lote hilo  kwa  muda  mrefu  haukuwa ukiangaliwa  kama  ilivyokuwa katika  vita  nchini  Syria. Lakini vita  vya  mataifa  mengine vinavyopiganwa  nchini  Libya, ni mzozo  wa  muda  mrefu.

Serikali  ya  Ujerumani ilianzisha juhudi za  kupambana na  hali hiyo, na  kuyaita  mataifa yenye  ushawishi  na  nguvu katika  mkutano  wa  Berlin, kuweza  kuzungumzia  kwa  uwazi, pamoja  na  utendaji, kuweza kuwaleta  pamoja  viongozi wanaopambana nchini  Libya kwa ajili  ya  upatanishi, hususan kuzuwia mtandao wa  kimataifa unaounga  mkono  vita, upelekaji wa  silaha na  kujinufaisha kiuchumi.

Bila  ya  usaidizi  wa  kimataifa, kila kitu kingesimama,  si upande  wa  serikali  inayoungwa mkono  kimataifa  ama  mbabe  wa kivita  Haftar, kusingewezekana kuchukua  hatua.

Kwa Ujerumani  kujiingiza  katika hatua  za  kidiplomasia ilikuwa sahihi. Katika  nyakati  hizi  za siasa  kali  za  kizalendo, mpango huo binafsi  unatambulika  na Umoja  wa  Mataifa  kuwa  ni suluhisho  halisi  la  Libya. Sasa hatua  ya  kusitisha  mapigano na  jumuiya ya  kimataifa kuangalia  usitishaji  huo vinaweza  kupatikana pamoja  na utimizaji  wa masharti ya  vikwazo vya  silaha  vya  Umoja  wa Mataifa.