1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Majaji wa Kifaransa wawasili Rwanda kuhusu mauaji ya kiholela

24 Novemba 2009

Yaonesha kana kwamba upepo wa kutoka Ulaya unaanza kuwakumba washukiwa wa mauaji ya kiholela ya Rwanda.

https://p.dw.com/p/KeJG
A young Rwandan girl walks through Nyaza cemetery outside Kigali, Rwanda Monday Nov. 25, 1996 where thousands of victims of the 1994 genocide are buried. Rwanda has claimed that virtually all the Rwandan refugees who fled to eastern Zaire in 1994 returned home last week. The refugees had fled Rwanda to escape retaliation for a Hutu-led massacre of half a million minority Tutsis. (AP Photo/Ricardo Mazalan
Makaburi ya wahanga wa mauaji ya kiholela nchini Rwanda mwaka 1994Picha: AP

Baada ya Ujerumani kuwatia mbaroni karibuni Wa-Nyarwanda wawili wanaoshukiwa kwa mauaji ya halaiki, ubakaji na uporaji katika eneo la mpaka wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na Rwanda, hivi sasa wamewasili mjini Kigali majaji wawili wa Kifaransa kufanya uchunguzi dhidi ya washukiwa wakubwa wanne, ambao wanatuhumiwa na wakuu wa Rwanda kuhusika na mauaji ya kiholela katika nchi hiyo. Majaji hao wa Kifaransa, Michele Ganascia na Fabinene Puos, hadi sasa hawajawaambia lolote waandishi wa habari. Othman Miraji punde hivi alizungumza na mwendeshaji mkuu wa mashtaka wa Rwanda, Martin Ngoga, kutaka kujua zaidi juu ya shughuli za Wafaransa hao hapo Kigali:

Mtayarishaji: Othman Miraji

Mpitiaji: Mohamed Abdulrahman