1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mahdi azuiliwa kurejea Misri

Sekione Kitojo
2 Julai 2018

Maafisa katika uwanja wa ndege wa Cairo walimzuwia kiongozi mkuu wa upinzani wa Sudan, Sadiq al-Mahdi, ambaye amekuwa akiishi uhamishoni nchini Misri kwa miaka kadhaa sasa. 

https://p.dw.com/p/30fdV
Sadiq al-Mahdi verhaftet
Picha: Hamid/AFP/Getty Images

Chama cha Umma kinachoongozwa na Mahdi kimesema vyombo vya usalama vilimzuwia waziri mkuu huyo wa zamani wa Sudan kuingia Misri wakati akirejea kwenye mkutano wa upinzani mjini Berlin, Ujerumani.  

Mahdi, ambaye amekuwa akiishi mjini Cairo, alisafiri kwenda London na mwanawe wa kike, Mariam, pamoja na msaidizi  wake.

Akihusika sana katika siasa nchini Sudan tangu miaka ya  1960, Mahdi alikuwa waziri mkuu kuanzia mwaka 1966  hadi 1967 na tena mwaka 1986 hadi 1989. 

Serikali yake ilikuwa ya mwisho kuchaguliwa kwa njia ya kidemokrasia nchini Sudan, kabla ya kuangushwa katika mapinduzi mwaka 1989 yaliyofanywa na rais wa sasa, Omar Hassan al-Bashir.