1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mageuzi makubwa kufanywa katika jeshi la Ujerumani

24 Agosti 2010

Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Karl-Theodor zu Guttenberg amewasilisha mapendekezo ya kufanywa mageuzi katika jeshi la Ujerumani "Bundeswehr."Hayo yatakuwa mageuzi makubwa kabisa katika historia ya jeshi la Ujerumani."

https://p.dw.com/p/OuXc
Verteidigungsminister Karl-Theodor zu Guttenberg (CSU), aufgenommen am Montag, 23. August 2010, im Paul-Loebe-Haus in Berlin. (apn Photo/Berthold Stadler)
Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani, Karl-Theodor zu Guttenberg.Picha: AP

Waziri Guttenberg amesema, anataka kupunguza idadi ya wanajeshi kwa theluthi moja yaani kutoka 250,000 hadi kama 163,000. Vile vile amependekeza kuondoa utaratibu wa kuandikisha wanajeshi kwa mujibu wa sheria, lakini amesema, sheria hiyo isiondoshwe bali iendelee kubakia katika katiba ya nchi. Kwa kufanya mageuzi hayo, jeshi litapunguza gharama zake na litakuwa na vikosi vilivyoandaliwa bora zaidi kwa operesheni zake na bila ya kuhatarisha usalama wa ndani alieleza waziri wa ulinzi Karl-Theodor zu Guttenberg.

Mwandishi: P.Martin/ZPR