1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mabingwa wa Afrika Nigeria wako ngangari

9 Juni 2014

Nigeria haikuwa na maandalizi mazuri ya Kombe la Dunia nchini Brazil 2014 na hata meneja Stephen Keshi ni mmoja wa wasiojuwa kinachoweza kutarajiwa kutoka kwa Super Eagles.

https://p.dw.com/p/1CF47
Interaktiver WM-Check 2014 Mannschaft Nigeria
Picha: picture alliance/augenklick

Mgogoro kuhusu marupurupu uliyagubika maandalizi ya Kombe la Mashirikisho mwaka wa 2013 na kisha Super Eagles wakabanduliwa nje ya duru ya kwanza ya dimba hilo.

Mabingwa hao wa Afrika Nigeria walirejea tena na kuwapiku Ethiopia katika mechi za mchujo ili kujikatia tikiti ya kwenda Brazil. Huku wakishiriki Kombe la Dunia kwa mara yao ya tano, nahodha wa Nigeria kwa mara nyingine atakuwa kungo nyota wa Chelsea John Obi Mikel. Nchi hiyo ina matarajio mengi kumhusu mchezaji Sunday Mba, anayecheza ligi ya nyumbani.

Watalaamu wengi wanaiona Nigeria kuwa timu yenye vipaji vingi barani Afrika na ambayo inaweza kuwaduwaza miamba wa Amerika ya Kusini na Ulaya. Lakini Super Eagles pia wanafahamika kwa ukosefu wa nidhamu uwanjani. Nigeria wamepangwa katika kundi F pamoja na Argentina, Iran na Bosnia- Herzegovina.

Mwandishi: Bruce Amani/dpa
Mhariri: Yusuf Saumu