1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

LOS ANGELES.mioto bado yawaka California

25 Oktoba 2007
https://p.dw.com/p/C7Cv

Watu zaidi ya nusu milioni wametakiwa wazihame nyumba zao ili kuepuka mioto inayoendelea kuwaka katika sehemu kadhaa za jimbo la California nchini Marekani.

Gavana wa jimbo hilo amearifu kwamba watu watatu wamekufa . Watu wengine 40 wamejeruhiwa na nyumba 1500 zimeungua.

Rais Bush anaetarajiwa kuwasili California leo ili kuona kiwango cha madhara amelitangaza jimbo hilo kuwa la maafa.