1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

London. Malkia awaonya wanaotaka kutumia dini vibaya.

31 Oktoba 2007
https://p.dw.com/p/C7Ay

Mfalme Abdullah wa Saudi Arabia amekutana na waziri mkuu wa Uingereza Gordon Brown leo kujadili masuala ya ugaidi, amani ya mashariki ya kati , pamoja na mkwamo kuhusu mpango wa kinuklia wa Iran kama sehemu ya ziara yake ambayo imeleta upinzani mkubwa.

Mfalme Abdullah ambaye pia ni waziri mkuu , ameishutumu Uingereza kwa kutofanya juhudi zaidi kupambana na ugaidi.

Akizungumza na malkia wa Uingereza mwanzoni mwa ziara yake jana , malkia amesema kuwa mataifa duniani yanapaswa kuwa pamoja ili kupambana na watu wanaotaka kutumia dini vibaya.

Brown ameieleza Saudi Arabia kuwa ni mshirika muhimu katika mashariki ya kati. Hii ni ziara ya kwanza kwa kiongozi huyo wa taifa la Kiislamu katika miongo miwili.