1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

LONDON : Kumbukumbu ya miaka 10 ya kifo cha Diana

1 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBTt

Misa ya kumbukubu kwa marehemu Princess Diana wa Uingereza imefanyika mjini London hapo jana.

Kumbukumbu hiyo ya miaka 10 ya kifo chake imehudhuriwa na wanawe wa kiume Prince William na Prince Harry ambao walioongoza mkusanyiko wa waumini wageni waalikwa 500 katika kanisa dogo karibu na Kasri la kifalme la Buckingham.

Miongoni mwa waliohudhuria kumbukumbu hiyo ni pamoja na mume wa zamani wa Diana Prince Charles,Waziri Mkuu wa Uingereza Gordon Brown,Mawaziri Wakuu wa zamani Tony Blair na John Major.