Liverpool walazimishwa sare, United na City watabasamu
27 Januari 2020Matangazo
Wakati huo huo United waliambulia ushindi wa sita bila walipokuwa ugenini kucheza na Tranmere.
Liverpool walikuwa wanacheza na Shrewsbury Town na kocha Jurgen Klopp alifanya mabadiliko mengi katika kikosi chake na mechi hiyo ikaishia sare ya mabao mawili kwa mawili. Sasa Liverpool watalazimika kucheza mechi ya marudiano na Shrewsbury uwanjani Anfield ingawa Klopp amesema hata katika mechi hiyo ya marudiano hatokichezesha kikosi chake cha kwanza kwani wachezaji hao wanastahili kupumzika.
Usiku wa Jumatatu AFC Bournemouth watakuwa wanawakaribisha Arsenal katika mechi nyengine ya kinyang'anyiro hicho cha FA Cup.