1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ligi ya Mabingwa Ulaya yaendelea kutimua vumbi

Bruce Amani
24 Februari 2020

Manchester City wamepigwa marufuku kushiriki mashindano ya Champions League kwa misimu miwili ijayo lakini kwa sasa wanalenga kutinga robo fainali ya mashindano ya msimu huu wakati watashuka dimbani dhidi ya Real Madrid

https://p.dw.com/p/3YKJg
UEFA Champions League 2019/20 | Schachtar Donezk vs. Manchester City
Picha: Reuters/G. Garanich

Manchester City wamepigwa marufuku kushiriki mashindano ya Champions League kwa misimu miwili ijayo lakini kwa sasa wanalenga kutinga robo fainali ya mashindano ya msimu huu wakati watashuka dimbani siku ya Jumatano na Real Madrid katika hatua ya 16 za mwisho.

Itakuwa mechi ya kwanza ya City tangu walipopigwa marufuku na UEFA kwa kukiuka sheria za usawa wa kifedha lakini wanasema watakata rufaa katika mahakama ya Usuluhishi michezoni.

Barca kwa upande wao watakwenda Napoli kesho Jumanne, zikiwa ni mechi za kwanza kabisa kwa makocha wa timu hizo, na katika siku hiyo, Bayern watawatembelea Chelsea katika mtanange wa marudio wa fainali ya 2012 ambayo Chelsea walishinda kwa penalty mjini Munich. Mechi nyingine ya Jumatano ni Juventus yake Cristiano Ronaldo dhidi ya Wafaransa Olympique Lyon.