1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Leverkusen yatinga nusu fainali ya Europa League

7 Agosti 2020

Bayer Leverkusen bila  matatizo  imewasili  katika  nusu  fainali  ya kombe  la  ligi ya  Ulaya , Europa league. Timu  hiyo  kutoka  katika Bundesliga Alhamis usiku iliishinda Glasgow rangers kwa  bao 1-0

https://p.dw.com/p/3gaZQ
Fußball Europa League Bayer Leferkusen - Glasgow Rangers
Picha: Getty Images/AFP/S. Schürmann

Bayer Leverkusen bila  matatizo  imewasili  katika  nusu  fainali  ya kombe  la  ligi ya  Ulaya , Europa league. Timu  hiyo  kutoka  katika Bundesliga Alhamis usiku iliishinda Glasgow rangers kwa  bao 1-0  na inaingia siku  ya  Jumatatu  katika  kinyang'anyiro cha  fainali  ya mashindano  hayo  mjini Dusseldorf  dhidi  ya  Inter Milan ya  Italia.

Eintracht  Frankfurt  pia  ya  Ujerumani imeyaaga  mashindano  hayo katika  awamu  ya robo  fainali katika  mchezo wa  mkondo  wa  pili dhidi  ya  FC Basel  ya  Uswisi  baada ya  kipigo cha  bao 1-0.

Mchezo wa  kwanza  kabla  ya  mapumziko  yaliyolazimishwa  na janga  la  cirusi  vya  corona  mwezi Machi Eintracht Frankfurt ilipoteza  mchezo  huo kwa  kuchapwa  mabao 3-1.