1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kuzorota kwa hali ya usalama Uganda nani wa kulaumiwa?

Sylvia Mwehozi
10 Septemba 2018

Wakati Uganda ikiendelea kukumbwa na hali mbaya ya  usalama na ya kisiasa, rais Museveni ameyalaumu mataifa ya kigeni kwa kuingilia masuala ya nchi hiyo yakifahamu kuwa ina inakaribia  kuwa na uchumi na usalama imara.

https://p.dw.com/p/34bRf
Uganda Polizeichef Muhammad Kirumira in Kampala
Picha: Getty Images/AFP/STRINGER

Museveni amesema kwamba serikali yake inaendelea kuimarisha usalama lakini inatatizwa na makundi ya watu wasioitakia mema  Uganda mema yakiwemo mashirika yasio ya kiserikali, vyombo vya habari na wengine ambao wanawachochea wananchi kujenga hisia potofu dhidi ya utawala wake..

Akihutubia taifa usiku wa wa kumkia Jumatatu , rais Museveni amevilaumu pia vyombo vya habari kwa kusambaza kile alichokiita  habari potofu kuhusu Uganda. Rais Museveni hata hivyo  amekiri kuwa hali ya usalama inazidi kuzorota na atachukua hatua ya kuwarudisha askari wa mgambo.

Kwa upande mwengine raia wengi wamelezea kutoridhishwa kwao na mikakati yake kwani amekuwa akisema yaleyale wakati mauaji ya kikatili yanapotokea,  kama vile  ilivyokuwa mwishoni mwa juma lililopita  wakati  afisa wa polisi maarufu Muhamad Kirumira alipopigwa risasi na kuuwawa  nje ya nyumbani kwake Jumamosi jioni.

Uganda Präsident Yoweri Museveni
Rais wa Uganda Yoweri Museveni Picha: picture-alliance/dpa/I. Langsdon

Mwishoni mwa wiki iliopita, Kulizuka mchanganyiko wa maoni, hofu na hasira miongoni mwa raia kufuatia mauaji ya afisa maarufu wa polisi Muhamad Kirumira  kukiwa na madai huenda  polisi ilikuwa baada ya marehemu kueleza kwamba maafisa wenzake walishirikiana na magenge ya wahalifu.

Siku ya Jumapili rais Museveni alitangaza hatua kadhaa za kupambana na kile amnbacho kwa wengi wanakiona kuwa ni  kuzorota kwa hali ya  usalama. Ameagiza kuandikishwa  kwa walinzi wa vijiji 24,000 ili kuisaidia  polisi kupambana na uhalifu.

Katika hotuba yake kwa taifa, Museveni alisisitiza kuwa kamwe hatoruhusu watu ambao hawajui jinsi Uganda ilivyopata amani , kuivuruga amani hiyo .

Mwandishi: Lubega Emmanuel

Mhariri. Mohammed Abdul-Rahman