1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kuwarejesha Waafghanistan ni kinyume na haki za binadamu

Sekione Kitojo
6 Oktoba 2017

Mataifa ya Umoja wa Ulaya yanatoa mbinyo kwa wakimbizi wa Afghanistan, ili warejea kwao kwa kile wanachosema kuwa ni kwa hiari yao, linasema shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International.

https://p.dw.com/p/2lJps
Deutschland Protest gegen Sammelabschiebung nach Afghanistan in Düsseldorf
Picha: picture-alliance/dpa/B. Thissen

Hii ni kinyume  na  sheria  anaeleza mtafiti wa shirika hilo la haki za binadamu  Horia Mosadiq  katika  mahojiano  yaliyofanywa  na  Jawad Amanullah  wa  DW.

Ripoti  ya   hivi  karibuni  kabisa  ya  Amnesty  International  inasema kuwa watu  nchini  Afghanistan  wanakabiliwa  na  matumizi  ya  nguvu, kutekwa  nyara  na  mauaji. Ni  hali  mbaya  kiasi  gani  inalikumba  jimbo la  Hindukush? aliulizwa  mtafiti  huyo Horia Mosadig, ambaye amesema, hakuna  usalama  nchini  Afghanistan.

Deutschland Protest gegen Sammelabschiebung nach Afghanistan in Düsseldorf
Wakimbizi wa Afganistan wakiandamana nchini UjerumaniPicha: picture-alliance/dpa/B. Thissen

Ametoa  mfano kwamba, alitekwa  nyara  baba  mmoja  wa  familia  na  watu  waliokuwa na  silaha, na  familia  yake  ikalazimika  kukusanya  fedha  zao  za mwisho  ili  kumkomboa  mzee  wao. Baada  ya  hapo  familia  hiyo ilikimbilia  Norway  na  kuomba  hifadhi  ya  ukimbizi.

Wakiwa  nchini  Norway  ombi  lao  la  hifadhi  ya  ukimbizi  lilikataliwa. Wakalazimika  kurejeshwa  nchini  Afghanistan. Miezi  michache baadaye  baba  huyo  alipotea  tena. Lakini  siku  chache  baadaye mwili  wake  ulionekana  mjini  Kabul  akiwa  amekufa. Wakimbizi  hao kwa  mujibu  wa  maafisa   walirejea  kwa  hiari  yao  kutoka  Ulaya. Wanapaswa kutambua  kuwa  kuna  hatari  katika  nchi  zao.

Hadi leo  kuna  Waafghanistan 9,000 waliorejeshwa  nchini  humo kutoka  Ulaya. Wengine 80,000 wako  katika  hatari  ya  kurejeshwa. Mataifa  ya  Ulaya  yanaonesha  kwamba  kurejea  kwa  Waafghanistan nchini  mwao  ni  kwa  hiyari. Lakini  ukweli  ni  kwamba  si  kwa  hiyari. Wakimbizi  wa  Afghanistan  wanaelezwa, kwamba  kwa  njia  moja  au nyingine  watarejeshwa  tu  makwao na  kuna aina  mbili  tu  ya uwezekano. Ama  warejeshwe  bila  kupewa  msaada  wowote, ama watie  saini  fomu  ya  kurejeshwa  na  wapatiwe  msaada  wa  serikali, ili  kujenga  maisha yao mapya  nchini  Afghanistan.

Deutschland Protest gegen Sammelabschiebung nach Afghanistan in Düsseldorf
Wakimbizi wa Afghanistan wakiandamana Picha: picture-alliance/dpa/B. Thissen

Wakimbizi wa Afghanistan

Ni Mataifa gani huwarejesha zaidi wakimbizi wa Afghanistan makwao. Ujerumani  ni  moja kati ya nchi hizo, ikifuatiwa na Ugiriki, Norway, Sweden na  uingereza.  Pamoja  na  hayo  nchi zote  karibu  za  Ulaya huwarejesha wakimbizi wa  Afghanistan  makwao. Anmesty International  imesema  inafanya  mazungumzo  na  nchi hizi  zote za Ulaya  pamoja  na  Afghanistan  yenyewe. Mahitaji  yetu  kwa  nchi  za Ulaya , ni  kwamba  zisichukue  tena  hatua  za  kuwarejesha  wakimbizi wa  Afghanistan. Kwa  upande  wa  serikali  ya  Afghanistan  tunatarajia , kwamba  zisitoe  msaada  ili  kuweza  wakimbizi  hao  kurejeshwa nchini  humo.

Kuhusu  msingi  gani  ambao  unatumiwa  na  mataifa  ya  Ulaya kuwarejesha  wakimbizi  hao, mtafiti  wa  Amnesty International  Horia Mosadiq  anasema,  ni  vigumu  kuweza  kupambanua  vipengee  vya uamuzi  huo. Lakini  hatua  ambayo  inaleta  wasi  wasi  mkubwa, ni kwamba  idadi  ya  kukataliwa  maombi  katika   mataifa  ya  Ulaya imepanda  mno  hivi  karibuni, hususan  tangu mwezi  Februari  ambapo serikali  ya  Afghanistan  ilipotia  saini  makubaliano  kuhusu  wakimbizi na  Umoja  wa  Ulaya.

Düsseldorf Sammelabschiebung  nach Afghanistan
Wanaharakati wakijadiliana na polisi katika kambi ya wakimbizi nchini UjerumaniPicha: picture-alliance/dpa/B. Thissen

Hadi  leo  haijakuwa  wazi, ni  jimbo  gani  katika  Afghanistan  ni salama, na  lipi  si  salama. Bado  hali  haifahamiki  katika  mataifa  ya Ulaya.

Wakimbizi mashoga

Tunafahamu  kutoka  kwa  wakimbizi  wenyewe, amesema  mtafiti  huyo wa  Amnesty International , kwamba  kwa  wale  waliotoa  sababu  ya kwamba  wao  ni  mashoga  ili  kuomba  hifadhi , pia  wanarejeshwa. Hata  waliobadili  dini  na  kuwa  Wakristo  na  wengine  wengi  ambao wanafuatiliwa  nchini  Afghanistan  kutokana  na  msimamo  yao  ya kisiasa  ama  kidini, hawana  msaada  katika  mataifa  ya  Umoja  wa Ulaya.

Afghanistan Journalisten protestieren vor dem Sitz der UNHCR
Baadhi ya waandishi habari wa Afghanistan wakisubiri maombi yao ya hifadhi ya kisiasa katika mataifa ya UlayaPicha: Framarz Sina

Majimbo  kama  Kabul, Panjshir, Bamyan yanaonekana  kuwa  yana usalama. Lakini  huo  sio ukweli  ulivyo. Kabul kwa  mfano  ndio  mji mkuu  wa  Afghanistan, na  ndiko  kunakotokea  mashambulizi  mara kwa  mara. Hatukubaliani  katika  swala  hili  na  kile   mataifa  ya  Ulaya yanachofanya.  Nchini  Afghanistan  hakuna  kanda  ambayo  ina usalama, na  hakuna  eneo , ambalo unaweza  kuwarejesha  wakimbizi. Nchi  ambazo zinachukua  hatua  ya  kuwarejesha  wakimbizi zinakwenda  kinyume  na  haki  za  binadamu.

Mwandishi: Amanullah, Jawad / ZR / Sekione  Kitojo

Mhariri: Josephat Charo