Lugha ya Kiswahili inazidi kusambaa ulimwenguni na kuwavutia watu wa mataifa kadhaa kuisoma na kuifanyia utafiti. Mmoja wao ni raia wa China, Yuning Shen, ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Hamburg, anakofanya utafiti kuhusu ghala la maneno ya Kiswahili kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter.