1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kundi la G7 lataka majibu kuhusu vita vya Iran

27 Machi 2026

Washirika wa mataida 7 yaliyoendelea kiviwanda duniani G7, wamemshinikiza Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani Marco Rubio, kuelezea mipango ya Marekani dhidi ya Iran.

https://p.dw.com/p/5BHQw
G7-Außenministertreffen 2026 | Arbeitssitzung zum Ukraine-Krieg mit Partnerländern
Kundi la G7 lataka majibu kuhusu vita vya Iran huku likiwa na wasiwasi kuhusu uhusiano wa Urusi na Jamhuri hiyo ya kiislamuPicha: Alain Jocard/AFP

Hayo yamejiri wakati kukiwa pia na wasiwasi wa uhusiano wa Urusi na Jamhuri hiyo ya kiislamu.

Kwa upande wake Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Johann Wadephul  amesema Jumuiya ya Kimataifa inahitajika kushirikiana kwa ukaribu zaidi kwa sasa wakati inaposhughulikia vita vya aina mbili, akimaanisha vita vya Urusi na Ukraine ambayvo amedai Urusi na Iran inashirikiana kuvitekeleza.

Kwengineko waziri wa mambo ya nchi za nje wa Uingereza Yvette Cooper amesisitiza kwamba kundi la G7 lina wasiwasi kuhusu mafungamano ya Urusi na Iran  baada ya ya nchi za Magharibi kuituhumu Moscow kuisaidia Tehran kushambulia vituo vya Marekani katika eneo la Ghuba.

Urusi imekanusha vikali tuhuma hizo.