1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kongamano la London la Wazanzibari walio ng'ambo

16 Desemba 2008

Kongamano juu ya mustakbali wa Zanzibar

https://p.dw.com/p/GFAP
Mji mkongwe wa ZanzibarPicha: DW /Maya Dreyer

Mjini London hii leo kunafanyika kongamano la mustakbali wa Visiwa vya Zanzibar lililoitishwa na jumuiya MUWAZA ambayo imesema madhumuni yake ni kuwaleta Wazanzibari pamoja kutoka ndani na nje ya nchi wajadili mambo yanayohusu nchi yao, kama vile Muungano wa Tanzania, haki za Zanzibar na kuiletea Zanzibar maendeleo. Mwenzangu Othman Miraji alizungumza kwa njia ya simu na Dr. Yusuf Saleh Salim, mmoja wa waasisi wa jumuiya ya Mustakbali wa Zanzibar, MUWAZA, kuhusu kongamano hilo: