Kongamano la London la Wazanzibari walio ng'ambo
16 Desemba 2008Matangazo
Mjini London hii leo kunafanyika kongamano la mustakbali wa Visiwa vya Zanzibar lililoitishwa na jumuiya MUWAZA ambayo imesema madhumuni yake ni kuwaleta Wazanzibari pamoja kutoka ndani na nje ya nchi wajadili mambo yanayohusu nchi yao, kama vile Muungano wa Tanzania, haki za Zanzibar na kuiletea Zanzibar maendeleo. Mwenzangu Othman Miraji alizungumza kwa njia ya simu na Dr. Yusuf Saleh Salim, mmoja wa waasisi wa jumuiya ya Mustakbali wa Zanzibar, MUWAZA, kuhusu kongamano hilo: