Kocha wa Barca akanusha ripoti za mvutano kikosini
29 Juni 2020Matangazo
Kocha wa Barca Quique Setien amesisitiza kuwa uhusiano wake na wachezaji ni mzuri, licha ya ripoti kuwa kuwepo ugomvi kikosini na mvutano kati ya Lionel Messi na naibu wa Setien, Eder Sarabia. "Uhusiano tulio na wachezaji ni mzuri. Ni kweli kwamba wakati mwingine ambapo mtu hukubaliana au kutokubaliana na kitu, lakini sioni tatizo lolote ambalo ni la kuzungumzia." Amesema Setien
Kulizuka majibizano baada ya sare ya 2 – 2 ya Barcelona na Celta Vigo matokeo yaliyowaweka Real Madrid kuchukua usukani na pengo la pointi mbili kwa kuwafunga Espanyol 2 – 0.
Msukosuko huo unakuja wakati mbaya ikizingatiwa kuwa Barca wanawaalika Atletico Madrid kesho Jumanne na hawahitaji kuteleza tena.