1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Klabu ya Zamalek kuadhibiwa baada ya kutofika uwanjani

Sylvia Mwehozi
26 Februari 2020

Shirikisho la soka nchini Misri EFA  limeahidi kuchukua hatua  baada ya mafahali  wa  mjini Cairo Zamalek kushindwa  kufika  katika  mchezo  wa  watani  wa  jadi jana dhidi ya mahasimu wao  wakubwa  Al Ahly mjini Cairo. 

https://p.dw.com/p/3YS93
CAF Super Cup 2020 in Katar ES Tunis - Zamalek
Picha: Getty Images/AFP/K. Jaafar

Shirikisho  la  kandanda  nchini  Misri EFA  limeomba  radhi kwa  mashabiki  baada  ya  mchezo  huo  kufutwa  na kusema  katika  taarifa  leo  kuwa  sheria  zake  za kinidhamu zitatumika. Zamalek  haikuwasili  uwanjani  kwa ajili  ya  mchezo  huo  ikipinga  dhidi  ya  vikwazo  vikali vilivyotolewa  dhidi  ya  wachezaji  wake  na  maafisa kutoka  vilabu  hivyo  viwili baada  ya   kupigana  wakati timu  hizo  zilipokutana  mjini  Abu Dhabi wiki  iliyopita katika   mpambano  wa  kombe  la  Super Cup. 

Rais  wa  Zamalek  Mortada Mansour  ni  miongoni  mwa wale  walipigwa  faini  na  amepigwa  marufuku  baada  ya mchezo   huo, ambao  walishinda  kwa  mabao 4-3 kupitia mikwaju  ya  penalti  baada  ya  kutoka  sare  bila kufungana.