1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUganda

Kiongozi wa upinzani Uganda atangaza kuondoka nchini

15 Machi 2026

Katika ujumbe uliotolewa Jumamosi, Bobi Wine alisema kuwa vikosi vya usalama viliweka vizuizi vya barabarani na kufanya msako ili kujaribu kumtafuta.

https://p.dw.com/p/5AQLQ
Uganda Kampala 2026 | Kiongozi wa upinzani Bobi Wine wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu uchaguzi wa rais
Kiongozi wa upinzani Uganda Bobi WinePicha: Rian Cope/AFP/Getty Images

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Bobi Wine, ametangaza kuwa ameondoka nchini humo baada ya kujificha kwa karibu miezi miwili tangu kumalizika kwa uchaguzi wa rais uliofanyika Januari.

Katika video iliyochapishwa kwenye mtandao wa kijamii wa X, Bobi Wine, ambaye jina lake halisi ni Robert Kyagulanyi, amesema amelazimika kuikimbia Uganda kwa muda kwa sababu ya vitisho vya usalama baada ya uchaguzi huo. Hata hivyo hakufahamisha mahala alipo.

Uchaguzi wa Januari 15 ulimrejesha madarakani rais wa muda mrefu wa Uganda, Yoweri Museveni, mwenye umri wa miaka 81, kwa muhula wa saba. Upinzani unasema matokeo ya uchaguzi huo yalijaa udanganyifu, madai ambayo serikali imekanusha.

Bobi Wine pia amesema akiwa nje ya nchi atafanya kampeni kimataifa ili kushinikiza vikwazo dhidi ya serikali ya Yoweri Museveni.

Ameongeza kuwa atarejea nchini siku zijazo, akisema kugombea urais si kosa la jinai.