KINSHASA: Watu takriban 17 wauwawa
28 Mei 2007Matangazo
Watu takriban 17 wameuwawa kwa kupigwa au kukatwakatwa na watu wanaotuhumiwa kuwa waasi wa Rwanda kwenye mkoa wa Kivu Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Inaripotiwa kwamba watu wengine yapata 30 walijeruhiwa na madarzeni kadhaa wakatekwa nyara wakati waasi hao walipovivamia vijiji viwili mnamo juzi Jumamosi.