Kifo cha msichana Mahsa Amini huko Iran bado kinachochea hamaki na hasira miongoni mwa umma wa taifa hilo. Mahsa alipoteza maisha akiwa chini ya mikono ya polisi kwa madai ya kutovaa kwa heshima. Maelfu bado wanaandamana kulaani kifo chake na kuonesha ghadhabu kwa utawala wa nchi hiyo.