1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

kazi kubwa yamsubiri Rouhani Iran

17 Juni 2013

Wairan wanapenda maajabu. Taifa hilo linaishangaza jamii yake, na jamii inaushangaza uongozi na wote huishanza jamii ya kimataifa. Hufanya hivyo kila wakati, na hata hivi karibuni katika uchaguzi wa rais nchini humo.

https://p.dw.com/p/18qxP
epa03746243 Thousands of supporters of newly elected President Hassan Rowhani take part during a street festivities right after the official announcement of his victory, in Tehran, Iran, 15 June 2013. Reformist candidate Rowhani has won Iran's presidential election with more than 50 percent of votes, outclassing the other five candidates. After eight years of hardliner Mahmoud Ahmadinejad, the new president Rowhani is likely to bring about a real change in both domestic and foreign policy. EPA/ABEDIN TAHERKENAREH
Uchaguzi wa Iran 2013Picha: picture-alliance/dpa

Kwa  mujibu  wa  baraza  la  ushauri  nchini  Iran  karibu  asilimia  99  ya wagombea  wa  uchaguzi  waliondolewa  na  kuacha  nafasi  finyu  ya kuweza  kuleta  mshangao,  baada  ya  kubakia  wagombea  sita   tu katika  uchaguzi  huo. Hassan Ruhani  mwenye  msimamo  wa  wastani pamoja  na  wagombea  wengine  watano  wahafidhina  waliingia  katika kinyang'anyiro  hicho  cha  kuwania  madaraka.

Hakuwapo  mgombea  ambaye  ni  maarufu  miongoni  mwa  wahafidhina waliogombea  uchaguzi  huo , na  Ruhani  alikuwa  hafahamiki sana. Kwa  hiyo  mtu  angetarajia  kuwa  uchaguzi  huo  ungeingia katika  duru  ya  pili,  kwa  kiasi  kikubwa  baina  ya  wagombea  wawili wahafidhina. Na  ghafla  kila  kitu  kikaenda tofauti kabisa.

epa03746244 Thousands of supporters of newly elected President Hassan Rowhani take part during a street festivities right after the official announcement of his victory, in Tehran, Iran, 15 June 2013. Reformist Rowhani has won Iran's presidential election with more than 50 percent of votes, outclassing the other five candidates. After eight years of hardliner Mahmoud Ahmadinejad, the new president Rowhani is likely to bring about a real change in both domestic and foreign policy. EPA/ABEDIN TAHERKENAREH
Wairan wakishangiria ushindi wa Rouhani katika uchaguzi wa raisPicha: picture-alliance/dpa

Uchaguzi  wa  rais  nchini  Iran  umeamuliwa   katika  duru  ya  kwanza tu.

Zoezi la  kuhesabu kura

Zoezi  la  kuhesabu  kura  lilikawia  kuliko  ilivyopangwa.  Shauku ilikuwa  inapanda  kila  dakika, hadi  pale  wizara  ya  mambo  ya  ndani nchini  Iran  ilipotoa  rasmi  matokeo  ya  uchaguzi  huo.

Hakuna  mtu  aliyefikiria  kuwa  Ruhani  angepata  ushindi  mkubwa  na usio  na  shaka  namna  hiyo.

Hali  hii  iliwezekanaje  basi?

An Iranian woman holds her purple scarf, the campaign color of moderate presidential candidate Hassan Rowhani, as she celebrates along Valiasr street after he was elected as president on June 15, 2013, in the capital Tehran. Rowhani, the cleric who won Iran's presidential election, is a moderate who has pledged to engage more with world powers in hopes of easing crippling economic sanctions. AFP PHOTO/BEHROUZ MEHRI (Photo credit should read BEHROUZ MEHRI/AFP/Getty Images)
Watu wa jinsia zote wamefurahia ushindi wa RouhaniPicha: Behrouz Mehri/AFP/Getty Images

Hali  ya  jamii  nchini  Iran  ni  mbaya kwa  kweli. Ukosefu  mkubwa  wa ajira, ughali  wa  maisha  unaopindukia  mipaka, uchumi  uliodumaa, vikwazo  vikali  na  mengi  mengine  yanaonekana   katika  maisha  ya kila  siku  katika  nchi  hiyo.

Na  juu  ya  hayo  linakuja  pigo  la  kisiasa , ambalo  lilitokana  na ukandamizaji  wa  vuguvugu  la  maandamano  baada  ya  uchaguzi  wa mwaka  2009.

Hali  kama  hiyo  ikiendelea  kwa  muda  mrefu  si  rahisi  kuizuwia  na huzaa  bila  shaka  hali  ya  kutoridhika , ambayo  inaakisi  matokeo  ya uchaguzi  huu.

Je ni  kura ya  maoni?

Matokeo  ya  uchaguzi  wa  rais  nchini  Iran  ni  kura  ya  kukataa kabisa  mpango  wa  kinuklia  pamoja  na  sera  za  mambo  ya  kigeni ya  wahafidhina  na  wakati  huo  huo  pigo  kwa   kiongozi  wa  kidini Ayatollah Ali  Khamenei.

Iranian moderate presidential candidate, Hassan Rowhani casts his vote at a polling station in Tehran on June 14, 2013 during the first round of the presidential election. Iranians are voting to choose a new president in an election the reformists hope their sole candidate will win in the face of divided conservative ranks, four years after the disputed re-election of Mahmoud Ahmadinejad. AFP PHOTO/ATTA KENARE (Photo credit should read ATTA KENARE/AFP/Getty Images)
Rais mteule wa Iran Hassan RowhaniPicha: AFP/Getty Images

Ndio  sababu  Hassan Ruhani  katika  muda  wa  chini  ya  wiki  moja amekuwa  mtu  anayebeba  matumaini  ya   wananchi  wa  nchi  hiyo, katika  kipindi  hiki  ambacho  wananchi  wamepoteza  matumaini. Tangu  siku  ya  kwanza  anakabiliana   na  changamoto  kubwa .

Anatakiwa  kwa  haraka  kutafuta  njia  ya  kuondoka  kutoka  katika mkwamo  wa  mazungumzo  ya  kinuklia, atafute  muafaka  na kubadilisha  sera  ambazo  hazina  tija  na  za  kuchochea  mambo. Ni kwa  njia  hiyo  tu  anaweza  kuwa  na  matumaini  ya  kuupooza  mzozo huo , ili kuweza  kulegezwa  vikwazo  na  pia  kuifanya   hali  ya  kijamii kuwa  bora  nchini  mwake.

Kwa  upande  mwingine  analazimika  kuongoza   upatanishi  na  jamii. Hali  hiyo  inawezekana  tu , iwapo  hatua  za  ukandamizaji  dhidi  ya jamii  zitasitishwa, wafungwa  wa  kisiasa  wataachiwa huru , hatua  za kuwekwa  kifungo  cha  nyumbani  kwa  mwanamageuzi  Mussawi pamoja  na  Karoubi  zitaondolewa , na   mbali  ya  hayo  uhuru  wa vyombo  vya  habari  pamoja  na uzuwiaji   upatikanaji  wa  taarifa utaondolewa.

Iran's Supreme Leader Ayatollah Ali Khamenei casts his ballot at his office during the Iranian presidential election in central Tehran June 14, 2013. Iranians voted for a new president on Friday urged by Khamenei to turn out in force to discredit suggestions by arch foe the United States that the election would be unfair. REUTERS/Fars News/Hassan Mousavi (IRAN - Tags: POLITICS ELECTIONS TPX IMAGES OF THE DAY) ATTENTION EDITORS - THIS IMAGE WAS PROVIDED BY A THIRD PARTY. FOR EDITORIAL USE ONLY. NOT FOR SALE FOR MARKETING OR ADVERTISING CAMPAIGNS. THIS PICTURE IS DISTRIBUTED EXACTLY AS RECEIVED BY REUTERS, AS A SERVICE TO CLIENTS
Kiongozi wa kidini wa Iran Ajatollah Ali KhameneiPicha: REUTERS/Fars News

Bila  shaka  kwa  kuchaguliwa  Ruhani  matarajio  ni  makubwa.   Mbali ya  kwamba  tunatambua   kuwa   njia  ya  malengo  hayo  ni   yenye mteremko  mkubwa  na  yenye  vikwazo  vingi.  Kwa  upande  mmoja kiongozi  wa  kidini , kuhusiana  na  masuala  muhimu  kama  suala  la kinuklia , ana  usemi  mkubwa. Kwa  upande  mwingine  wahafidhina katika  bunge  wana  nguvu  kubwa. 

Kwa  hiyo  ushindi  katika  uchaguzi wa  rais  ni  hatua  ya   kwanza. Matumaini  makubwa  yanaweza kuelekeza  katika  kuvunjwa  moyo  kukubwa,  watu  wa  Iran hilo wamekwisha  kuliona  mara  kwa  mara. Lakini  mara  hii, wakati  ni mfupi  mno  na  gharama  za  kuvunjika  tena  moyo  ziko  juu  mno.

Mwandishi: Jamsheed Faroughi / ZR /Sekione  Kitojo

Mhariri: Josephat Charo