1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Mafunzo

Karandinga: Maamuzi Mabaya

Grace Kabogo
4 Machi 2020

Wagonjwa wa kipinduindu wamekuwa wakiongezeka katika msimu wa mvua kwenye mji wa Magarya. Juhudi za kuutokomeza ugonjwa huo zinaendelea, ingawa zinakwamishwa kwa kiasi fulani.

https://p.dw.com/p/3YqXU
DW Crime Fighters Serienmotiv „Uneasy choices“

Mji wa Magarya na mkoa jirani mara nyingi inakabiliana na kuongezeka kwa wagonjwa wa kipindupindu wakati wa msimu wa mvua. Mwaka huu kuna hofu ya kutokea janga la kweli. Kwa bahati nzuri, fedha zimetengwa ili kusaidia kuzuia na kuimarisha miundombinu kabla mvua kubwa hazijaanza kunyesha. Marafiki Hajra, Karima na Sabitu, wanaojitolea katika Kituo cha Afya cha Jamii, wana shauku kubwa kuhusu wazo hilo… hadi Hajra alipoanza kushuku mwenendo wa meya ya Magarya. Ni kweli anataka kuwekeza fedha hizo kwa faida ya jamii? Au kuna kitu kingine kinaendelea? Kwa nini Aboubakar, mkuu wa Kituo cha Afya cha Jamii, amekuwa na tabia ya kushangaza? Lakini uchunguzi wa Hajra unaweza kumuweka matatani. Na mwaka wao wa kujitolea haraka unageuka kuwa jinamizi kwa marafiki hao watatu.

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi

Gundua zaidi

Onesha taarifa zaidi