Kansela wa Ujerumani ziarani Mongolia
13 Oktoba 2011Matangazo
Wakati wa ziara hiyo, Merkel anatazamiwa kutia saini mikataba inayohusika na malighafi atakapokutana na Rais Tsakhia Elbegdory na Waziri mkuu Sukhbaatar Barbold. Mikataba hiyo itahakikisha kuvipatia viwanda vya Ujerumani, madini yenye thamani kubwa ambayo uhitajiwa katika viwanda vya teknolojia ya hali ya juu ,ikiwa ni pamoja na viwanda vya kutengenezea simu za mkononi.
Kabla ya kuwasili Ulan Bator, Kansela Merkel alisema, Mongolia inajitahidi kuelekea kwenye demokrasia. Uchumi wa nchi hiyo kwa sehemu kubwa unategemea majirani wake Urusi na China. Merkel ni kansela wa kwanza wa Ujerumani kuizuru Mongolia nchi iliyo na wakaazi milioni tatu.