Vazi muhimu la Afrika
Kanga ni maarufu kwa michoro yake ya rangi za kuvutia ambayo mara nyingi huakisi maisha ya kila siku ya watu wa pwani. Michoro hiyo ni ya aina nyingi. Kuna nakshi tofauti pamoja na michoro ya ndege na maua. Kwa sasa, kanga maarufu zinapatikana katika nchi tofauti za Afrika Mashariki kama vile Tanzania, Kenya, Madagascar, visiwa vya Comoro, Msmbumbiji na Mashariki mwa DRC.