Kabul. Watu saba wauwawa na Taliban.
15 Oktoba 2006Matangazo
Mashambulizi kadha yanayohusishwa na wapiganaji wa Taliban nchini Afghanistan yamesababisha watu saba kuuwawa leo , wakati serikali ya Italia inasema kuwa inaamini mwandishi wa habari ambaye amepotea ametekwa nyara.
Hali hiyo ya machafuko inahusishwa na kundi la Taliban , lakini msemaji wa kundi hilo la waasi amesema kuwa kundi hilo halihusiki na kupotea kwa mwandishi habari huyo Gabriele Torsello.