1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KABUL: Shambulio la bomu limeua wanajeshi wa Kijerumani

19 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CC0e

Wanajeshi 3 wa Kijerumani na raia 4 wameuawa nchini Afghanistan.Kwa mujibu wa maafisa wa Afghanistan,mwanamgambo aliejitolea muhanga, alishambulia wanajeshi waliokuwa wakipiga doria katika wilaya ya kaskazini ya Kundus.Hadi watu 14 wengine pia walijeruhiwa katika shambulio hilo, wawili wakiwa ni wanajeshi wa Kijerumani.Kiasi ya wanajeshi 3,000 wa Ujerumani wapo kaskazini mwa Afghanistan,kama sehemu ya vikosi vya amani vya NATO nchini humo.