1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KABUL: Afisa mmoja wa polisi auwawa

23 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CBzG

Afisa mmoja wa polisi ameuwawa wakati mshambuliaji wa kujitoa muhanga maisha aliyekuwa kwenye pikipiki alipojilipua karibu na makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini Kabul. Watu wengine watano wamejeruhiwa kwenye shambulio hilo, wakiwemo maafisa wawili wa polisi.

Msemaji wa polisi amesema hujuma hiyo imefanywa katika mojawapo ya barabara zilizo na shughuli nyingi mjini Kabul.