Wasanii hasa wa muziki nchini Tanzania wamekuwa wakilalamikia utaratibu wa kuwasilisha tungo zao kwa uhakiki katika baraza la sanaa la BASATA kabla ya kutolewa kwa umma. Hoja wanazozitoa ni kwamba uhakiki huo sio tu unabana uhuru wao wa kutoa mawazo, bali pia unaweza kukwamisha sekta ya sanaa. Msikilize Daniel Gakuba akizungumza na kaimu mkurugenzi wa BASATA Matiko Mniko.