Kwa wanamuziki wengi wa kizazi kipya, lugha ya kuuzia kazi zao ni Kiswahili kinachochanganywa na maneno au madoido ya Kiingereza cha Marekani, lakini mwanamuziki wa Hip Hop kutoka Tanzania, Nash MC, anaamini muziki huo unaweza kuimbwa kwa Kiswahili Fasaha na bado ukawavutia wengi sana. Nash ndiye mgeni wetu leo kwenye Kiswahili Kina Wenyewe, akizungumza na Mohammed Khelef.